MWENYEMACHO DOT COM

Yanapojiri Nilipo na Wewe Upo

K-LYN NA WASHKAJI

Posted by Bob Sankofa on November 10, 2007

ntuyabaliwe2.jpg

Vyombo vya habari noma sana, huwa vinakuza watu kupita maelezo kiasi kwamba hata ukikutana na watu wale wanaokuzwa kivile unaweza ukaogopa hata kuwasalimia. K-Lyn, mwanamuziki wa kizazi kipya Bongo na ambaye pia amewahi kuwa Miss Tanzania, alikuwepo jana kwenye shughuli ya Redd’s. Basi nikajipitisha mara ya kwanza nikitaka kula snepu lakini nikasita kwa kuhofia kutolewa nishai, nikarudi mara ya pili nikatabasamu kidogo na yeye akatabasamu, sikuchelewa nikabaruza hii. Dada hana makuu kabisa, akanipa ruhusa ya kubaruza foto zingine kama tano hivi, nimeziweka maktaba kwa matumizi ya baadae.

Leave a comment