MWENYEMACHO DOT COM

Yanapojiri Nilipo na Wewe Upo

Archive for March, 2008

FATMA NA MAMBO YA FESTIVE COLLECTIONS

Posted by Bob Sankofa on March 7, 2008

sauti-day-3-146.jpg
Fatma Amour wa lebo ya mitindo ya Famour kesho usiku katika hoteli ya Move n Pick atafanya onesho la mitindo ya kazi zake alilolibatiza jina la Festive Collections. Wewe umepanga kwenda wapi kesho? Basi katika mitoko yako anza na huu. Njoo na shilingi elfu ishirini za kiingilio, uje kuona mambo mazito ya dada Fatma.
modelsbc.jpg
Hawa ni wanamitindo watakovaa nguo za Famour kesho pale hotel ya Move n Pick. Usikose kumuunga dada Fatma mkono.

Posted in Africa, Art, Bongo, Burudani, Fashion, Fotografia, Kazi, mitindo, Photography, Sanaa, Tanzania | 1 Comment »

SASA BAADA YA HAPA NINI KINAFUATA?

Posted by Bob Sankofa on March 7, 2008

picture-049_wafadhili.jpg

Abdi Simba, mmoja wa wamiliki wa taasis ya Flame Tree, waandaaji wakubwa wa maonesho haya akiongea jambo na mama wa Benki ya Kenya (mama aliyetoa pesa za ufadhili). Hapa nadhani mama alikuwa anamuuliza jamaa kuwa ana mpango gani baada ya onesho hili.

 Katikati ni mkurugenzi wa kampuni ya utayarishaji filamu ya Savannah na aliyewahi kuwa mkurungenzi mkuu wa Zanzibar International Film Festiva, Imruh Bakari.

Posted in Africa, Art, Bongo, Burudani, Fotografia, Kazi, Kimataifa, Photography, Sanaa, Tanzania | 1 Comment »

NYONGEZA YA MAONESHO

Posted by Bob Sankofa on March 7, 2008

picture-025_mauzo.jpg
Kama huna uwezo wa kununua sanaa (Vinyago) kubwa-kubwa za kina dada hawa basi unaweza ukanunua poster za moanesho haya kwa shilingi elfu tano au kwa kina mama unaweza kununua vifaa vya urembo vinavyotokana na miti kama bangili, hereni na mikufu. Ni namna fulani ya kujiwekea kumbukumbu kuwa ulihudhuria maonesho haya. Pili ndio alikuwa mezani jana.

Posted in Africa, Art, Bongo, Burudani, Fotografia, Kazi, Photography, Sanaa, Tanzania | 1 Comment »

UMECHEKI HIZI?

Posted by Bob Sankofa on March 7, 2008

picture-027_wageni.jpg
Baadhi ya wageni wachache wakiangalia baadhi ya kazi za kina dada wasanii wachongaji. Kazi zinafurahisha kwa kweli.

Posted in Africa, Art, Bongo, Burudani, Fotografia, Kazi, Photography, Sanaa, Tanzania | Leave a Comment »

KARIBU MGENI

Posted by Bob Sankofa on March 7, 2008

picture-010_karibu-mgeni.jpg

Mwandale Mwanyekwa, msanii na  muandaaji mshiriki wa maonesho haya akiwakaribisha wageni waliofanikisha uwepo wa maonesho haya kwa kutoa fedha. Mwenye nguo ya bluu ni mama kutoka Benki ya Kenya na huyo mzungu ni mfadhili toka Ubalozi wa Uswizi. Wafadhili hawa wameahidi mbele ya hadhira kwamba msaada wao hautaishia kwenye maonesho haya, watasaidia kina dada hawa kuanzisha chama cha Wasanii Wanawake Tanzania.

Dada mwenye mtoto pale nyuma ni Pili, msanii mshiriki, na yule mwenye kilemba cha buluu bahari ni Pudenciana, msanii mshiriki vilevile.

Posted in Africa, Art, Bongo, Burudani, Kazi, Kimataifa, Photography, Sanaa, Tanzania | 2 Comments »

MAONESHO YAKO WAZI

Posted by Bob Sankofa on March 7, 2008

picture-003_yamefunguliwa.jpg

Hatimaye yale maonesho ya Wasanii Wachongaji Wanawake wa Tanzania yamefunguliwa rasmi jana usiku. Hawa ni baadhi ya wageni waliofanikiwa kuwaunga mkono dada zetu. Maonesho yako wazi hadi tarehe 26 mwezi huu. Ukitoka kazini pita pale Makumbusho ya Taifa siku moja uone kinachoendelea.

Posted in Africa, Art, Bongo, Burudani, Fotografia, Kazi, Photography, Sanaa, Tanzania | Leave a Comment »

KILABU CHA USHAIRI CHAPATA UGENI

Posted by Bob Sankofa on March 5, 2008

img_0241_3_1.jpg
Jumanne ya mwisho ya mwezi wa uliopita kile kilabu chetu cha ushairi japa Bongo kilitembelewa na mwandishi mkubwa wa vitabu vya riwaya toka kule Afrika ya Kusini. Mwandishi huyu anakwenda kwa jina la Ms. Koenings. Wanachama walifurahia nafasi hiyo kwani waliweza kumuuliza mwandishi huyu maswali kadha wa kadha.
 img_0239_1_1.jpg
Koenings akisoma sehemu ya kitabu chake alichotoa hivi karibuni. Kitabu kinakwenda kwa jina la “The Blue Taxi”.
Picha kwa hisani ya kamera ya simu ya kiganjani ya Sandra Mushi.

Posted in Africa, Art, Bongo, Burudani, Elimu, Fotografia, Kazi, Kimataifa, Mikutano, Photography, Poetry, Sanaa, Tanzania | 1 Comment »

“MGUU SAWA ” KWA MAONESHO

Posted by Bob Sankofa on March 5, 2008

img_9177_mwandale2.jpg

Mwandale Mwanyekwa, msanii mwanamke wa fani ya uchongaji, akimalizia moja ya sanaa zake nyingi zitakazojiri pale katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa kuanzia siku ya Tarehe 7 asubuhi. Maonesho yanafunguliwa kesho usiku lakini watakaojiri kesho ni wale waliopewa kadi za mwaliko tu halafu kwa muda wa wiki tatu zijazo yatakuwa wazi kwa Watanzania wote. Kiingilio BURE.

img_9648_mwandale1.jpg

Sanaa inapakwa mafuta, nafikiri hii ni namna fulani ya kuongeza thamani ya sanaa hii maana baada ya kupakwa mafuta kazi hii huwa inang’ara kwelikweli.

Posted in Africa, Art, Bongo, Fotografia, Kazi, Photography, Sanaa, Tanzania | Leave a Comment »

WASANII WACHONGAJI WANAWAKE TANZANIA

Posted by Bob Sankofa on March 4, 2008

womensculpturepostersmall2.jpg
Tarehe 7 ya mwezi huu katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa kutakuwa na maonesho ya sanaa ya uchongaji wa vinyago. Maonesho yatadumu kwa muda wa wiki tatu, hiyo ni hadi tarehe 26 ya mwezi huu wa tatu. Karibu uwape sapoti kina dada. Wasanii wenyewe ni Mwandale Mwanyekwa, Pili Mtonga, Hawa Jarufu na Pudenciana Mwamalumbili. Kwa taarifa zaidi soma posters zilizosambazwa jiji zima, hadi kule visiswa vya karafuu nako wanazo habari pia. Kila la heri!

Posted in Africa, Art, Bongo, Fotografia, Kazi, Photography, Sanaa, Tanzania | 1 Comment »