MUGONGO MUGONGO YA PWANI!
Posted by Bob Sankofa on August 9, 2007
Ulishawahi kuona ndugu zetu wa visiwa vya karafuu wakiyarudi magoma ya pwani?
Video hii niliipiga kwenye mkutano wa TED pale Arusha mwezi wa sita mwaka huu. Wakinadada hawa ni wanenguaji wa Bi. Kidude, yule mkongwe wa muziki wa mwambao.
Nilikuwa nasikia tu kwamba muziki wa mwambao pia wanakata viuno balaa. Hebu shuhudia kwa macho yako mwenyewe jinsi wakina dada hawa na bendi lao wanavyolisakanyua jukwaa pale Ngurudoto Lodge.
UHURU!




