MWENYE MACHO AUZA PICHA YA KWANZA
Posted by Bob Sankofa on July 3, 2007
Hatimaye Mwenye Macho ameuza picha yake ya kwanza katika maisha yake ya upigaji picha kwenye jarida moja huko Ufaransa kupitia wakala wa picha aitwaye Cedric Galbe. Cedric Galbe ni mpiga picha wa Kifaransa ambaye ameanzisha tovuti iitwayo www.Galbe.com. Tovuti hii ni wakala wa wapiga picha toka Africa, Scandinavia, Mashariki ya Kati, na Marekani ya Kusini.
Picha aliyouza ni hiyo hapo juu ya mtaalamu wa hesabu aitwaye Ron. Ron alitoa mada kwenye mkutano wa TED uliofanyika Arusha mwezi uliopita. Mada yake ilikuwa inaonyesha ni kwa jinsi gani hesabu zinavyothibitisha kuwa maisha yalianzia Afrika. Kwa habari zake zaidi tembelea www.jikomboe.com, Ndesanjo alimwandika vizuri zaidi. Mimi sikumwelewa sawasawa kwani mimi na hesabu hatukuwahi kuwa marafiki hata kidogo.
Mpaka wakati mwingine, naelekea benki mara moja kuona kama dola zangu zimeingia.





mwandani said
babu kubwa. endeleza mapambano.
Jeff Msangi said
Hongera sana Sankofa,
Huu ni mfano mzuri na ushuhuda kwamba blogs sio tu chanzo cha habari bali pia utajiri.Endelea na mwendo huo huo.
Serina said
hongera.
ndesanjo said
hongera sana Sankofa
ndesanjo said
hongera sana Sankofa
Egidio Ndabagoye said
Kaka imetulia sana hii.Endeleza mapambano.
Bob Sankofa said
Nawashukuruni nyote, asanteni sana
Global Voices Online » Tanzania: Tanzania blogger sells photo from his blog said
[...] Tanzanian blogger, Sankofa, has sold a photo he posted on his blog from TEDGlobal 2007. Share [...]